Rais wa Syria
Bashar al Asaad ameapa kulikomboa taifa lote la Syria katika mahojiano
na kituo cha habari cha AFP saa chache tu baada ya makubaliano ya
kusitisha vita.
Ameiambia AFP kwamba kushiriki kwa mataifa mengine nchini Syria kunamaanisha suluhu itachakua muda mrefu.Awali ,Umoja wa mataifa ulisema kuwa unatumai kuanza kupeleka chakula katika maeneo yaliozungukwa katika kipindi cha saa 24.
Zaidi ya watu 250,000 wameuawa na zaidi ya milioni 11 kuwachwa bila makao katika mapigano ya miaka mitano nchini humo.
Baadhi ya miji kadhaa ya Syria imekatwa na haiwezi kupokea misaada kwa kiindi cha mwaka mmoja kutokana na vita.
Takriban watu milioni 13.5 wanahitaji msaada ,UN imesema.
CHANZO BBC.



No comments:
Post a Comment