Wakati Bastian Schweinsteiger, Matteo Darmian na Morgan Schneiderlin wakielekea Old Trafford kukamilisha ndoto zao za kujiunga na moja ya vilabu vikibwa duniani, Robin van Persie yeye ameondoka kwenye klabu hiyo.
Mshambuliaji huyo jana alisafiri kwenda Istanbul na alipokelewa kama mfalme na mashabiki wa klabu yake mpya.
“Nimekuja kujiunga na klabu nzuri na kubwa, ni heshima kubwa kwangu.” Alisema Van Persie.
Fenerbahce walithibitisha Alhamisi kwamba wameingia kwenye mazungumzo na United juu ya uhamisho wa ndachi huyo.
Van Persie sasa anaungana na mchezaji mwenzie wa zamani wa United, Luis Nani.
No comments:
Post a Comment